Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo ambapo mchezo mmoja kati ya KMC dhidi ya Namungo Fc utapigwa uwanja wa KMC Comlex, Kinondoni jijini Dar es salaam
Ni mechi itakayozikutanisha timu mbili ambazo zimezinduka zikitoka kushinda mechi zao zilizopita
KMC waliichapa Prisons mabao 2-1 katika mchezo uliopita wakati Namungo Fc ambayo inanolewa na kocha Juma Mgunda, iliichapa Pamba Jiji bao 1-0
Kama KMC itaibuka na ushindi katika mchezo huo unaweza kusogea hadi nafasi ya sita katika msimamo sasa ikiwa ya 9 ikikusanya alama 11
Namungo wameshinda mechi tatu tu msimu huu, wakishika nafasi ya 12 na alama zao 9



