Mashujaa watangaza viingilio mechi dhidi ya Simba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 31st October 2024


Mashujaa watangaza viingilio mechi dhidi ya Simba

Ijumaa, Novemba 01 Mashujaa Fc itakuwa mwenyeji wa mchezo wa ligi kuu dhidi ya Wekundu wa Msimbazi, Simba Sc ambao utapigwa uwanja wa Lake Tanganyika, saa 10 jioni

Mashujaa wametanga viingilio vya mchezo huo jana ambapo tiketi za VIP ni Tsh 30,000/-, majukwaa mengine ni Tsh 10,000/- na wale wa kusimama watalipa kiingilio cha Tsh 5,000/-

Simba iliondoka jijini Dar es salaam mapema leo, ikitarajiwa kutua Kigoma Alhamisi mchana

Kikosi cha kocha Fadlu Davids jioni kitapata nafasi ya kufanya mazoezi ya mwisho katika uwanja wa Lake Tanganyika


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.