Ijumaa, Novemba 01 Mashujaa Fc itakuwa mwenyeji wa mchezo wa ligi kuu dhidi ya Wekundu wa Msimbazi, Simba Sc ambao utapigwa uwanja wa Lake Tanganyika, saa 10 jioni
Mashujaa wametanga viingilio vya mchezo huo jana ambapo tiketi za VIP ni Tsh 30,000/-, majukwaa mengine ni Tsh 10,000/- na wale wa kusimama watalipa kiingilio cha Tsh 5,000/-
Simba iliondoka jijini Dar es salaam mapema leo, ikitarajiwa kutua Kigoma Alhamisi mchana
Kikosi cha kocha Fadlu Davids jioni kitapata nafasi ya kufanya mazoezi ya mwisho katika uwanja wa Lake Tanganyika




