Guardiola alia na majeruhi Man City

Joel JJ By Joel JJ β€’ 31st October 2024


Guardiola alia na majeruhi Man City

Mkufunzi wa Manchester City Pep Guardiola amesema wako matatani baada ya kupata majeraha zaidi walipochapwa 2-1 na Tottenham kwenye Kombe la Carabao na kuwaacha na wachezaji 13 pekee wa kikosi cha kwanza

Tayari bila Kyle Walker, Rodri, Oscar Bobb, Jeremy Doku, Kevin De Bruyne na Jack Grealish walikokosa mechi hiyo ya raundi ya nne]

Manuel Akanji alitolewa kabla ya mchezo kuanza huku Savinho akitolewa kwa machela kipindi cha pili

Mabao ya Timo Werner na Pape Sarr yakathibitisha kichapo cha kwanza kwa Guadiola msimu huu huku Mhispaniola huyo akikiri matatizo yameongezeka kabla ya mechi ya ligi Jumamosi dhidi ya Bournemouth, ambayo inafuatiwa na Ligi ya Mabingwa dhidi ya Sporting Lisbon

"Tuna wachezaji 13 (waliopo) kwa hivyo tuko kwenye shida sana. Wanaocheza, wanamaliza lakini wengi wao wana matatizo na tutaona jinsi wanavyopona," alisema


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.