Mkufunzi wa Manchester City Pep Guardiola amesema wako matatani baada ya kupata majeraha zaidi walipochapwa 2-1 na Tottenham kwenye Kombe la Carabao na kuwaacha na wachezaji 13 pekee wa kikosi cha kwanza
Tayari bila Kyle Walker, Rodri, Oscar Bobb, Jeremy Doku, Kevin De Bruyne na Jack Grealish walikokosa mechi hiyo ya raundi ya nne]
Manuel Akanji alitolewa kabla ya mchezo kuanza huku Savinho akitolewa kwa machela kipindi cha pili
Mabao ya Timo Werner na Pape Sarr yakathibitisha kichapo cha kwanza kwa Guadiola msimu huu huku Mhispaniola huyo akikiri matatizo yameongezeka kabla ya mechi ya ligi Jumamosi dhidi ya Bournemouth, ambayo inafuatiwa na Ligi ya Mabingwa dhidi ya Sporting Lisbon
"Tuna wachezaji 13 (waliopo) kwa hivyo tuko kwenye shida sana. Wanaocheza, wanamaliza lakini wengi wao wana matatizo na tutaona jinsi wanavyopona," alisema



