Klabu ya Azam Fc imethibitisha kumuongeza mkataba wa mwaka mmoja winga Abdul Suleiman Sopu
Mkataba wa Sopu na Azam Fc ulikuwa umalizike mwishoni mwa msimu huu lakini sasa winga huyo ataendelea kusalia Azam Fc hadi mwaka 2026
Sopu alianza vibaya msimu huu akipata majeraha ambayo yamemuweka nje ya uwanja kwa zaidi ya wiki sita



