Yanga yatangaza viingilio mchezo dhidi ya Azam Fc

Joel JJ By Joel JJ β€’ 31st October 2024


Yanga yatangaza viingilio mchezo dhidi ya Azam Fc

Mapema wiki hii Bodi ya Ligi Kuu ilitangaza mabadiliko ya uwanja ambao mchezo wa ligi kuu kati ya Yanga dhidi ya Azam Fc 'Dar es salaam Derby' mchezo huo ukihamishwa kutoka uwanja wa Benjamin Mkapa na kupelekwa Azam Complex sababu ikielezwa ni ukarabati unaoendelea katika dimba la Mkapa

Yanga ambao jana walikuwa Zanzibar kumenyana na Singida Black Stars na kuibuka na ushindi wa bao 1-0, wametangaza viingilio vya mchezo huo utakaopigwa saa 12 jioni

Mzunguuko ni Tsh 10,000/-, VIP B ni Tsh 30,000/- na VIP A ni Tsh 50,000/-

Baada ya uwanja wa Azam Complex kuwekwa viti, sasa uwanja huo unachukua chini ya mashabiki 7,000


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.