Mapema wiki hii Bodi ya Ligi Kuu ilitangaza mabadiliko ya uwanja ambao mchezo wa ligi kuu kati ya Yanga dhidi ya Azam Fc 'Dar es salaam Derby' mchezo huo ukihamishwa kutoka uwanja wa Benjamin Mkapa na kupelekwa Azam Complex sababu ikielezwa ni ukarabati unaoendelea katika dimba la Mkapa
Yanga ambao jana walikuwa Zanzibar kumenyana na Singida Black Stars na kuibuka na ushindi wa bao 1-0, wametangaza viingilio vya mchezo huo utakaopigwa saa 12 jioni
Mzunguuko ni Tsh 10,000/-, VIP B ni Tsh 30,000/- na VIP A ni Tsh 50,000/-
Baada ya uwanja wa Azam Complex kuwekwa viti, sasa uwanja huo unachukua chini ya mashabiki 7,000




