Wekundu wa Msimbazi, Simba Sc wako mkoani Kigoma ambapo leo walikamilisha maandalizi yao ya mwisho katika uwanja wa Lake Tanganyika kuelekea mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mashujaaa Fc utakaopigwa Ijumaa jioni
Kikosi cha Simba kiliwasili Kigoma majira ya mchana kikipata mapokezi makubwa kutoka kwa mashabiki wao
Na jioni wakatimiza taratibu za kinanuni kwa kufanya mazoezi katika uwanja ambao utatumika hapo kesho
Mashujaa Fc dhidi ya Simba ni mechi kubwa inayosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka mkoani Kigoma na maeneo ya jirani hapo kesho
Kumekuwa na tambo za kuibuka na ushindi kutoka kila upande lakini mwisho wa tambo hizo ni dakika 90 za mchezo huo utakaopigwa saa 10 jioni



