Simba yajifua Lake Tanganyika

Joel JJ By Joel JJ β€’ 31st October 2024


Simba yajifua Lake Tanganyika

Wekundu wa Msimbazi, Simba Sc wako mkoani Kigoma ambapo leo walikamilisha maandalizi yao ya mwisho katika uwanja wa Lake Tanganyika kuelekea mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mashujaaa Fc utakaopigwa Ijumaa jioni

Kikosi cha Simba kiliwasili Kigoma majira ya mchana kikipata mapokezi makubwa kutoka kwa mashabiki wao

Na jioni wakatimiza taratibu za kinanuni kwa kufanya mazoezi katika uwanja ambao utatumika hapo kesho

Mashujaa Fc dhidi ya Simba ni mechi kubwa inayosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka mkoani Kigoma na maeneo ya jirani hapo kesho

Kumekuwa na tambo za kuibuka na ushindi kutoka kila upande lakini mwisho wa tambo hizo ni dakika 90 za mchezo huo utakaopigwa saa 10 jioni


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.