Local,Normal News,Mashujaa, Simba

Hatumwi mtoto dukani Kigoma leo

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1 Nov 2024
Hatumwi mtoto dukani Kigoma leo

Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo ambapo mchezo mmoja unapigwa mkoani Kigoma. Mashujaa Fc watakuwa wenyeji wa Simba katika mchezo unaosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka nchini

Wekundu wa Msimbazi waliotua Kigoma jana, watashuka dimba la Late Tanganyika wakifahamu ushindi dhidi ya Mashujaa leo utawahakikishia kusogea nafasi ya pili katika msimamo wa ligi

Kocha Mkuu wa Simba, Fadlu Davids, amesema kikosi chake kipo tayari kwa ajili ya mchezo huo na malengo yao ni kupata pointi tatu ili kujiimarisha katika msimamo wa ligi hiyo

Fadlu amesema anatarajia mechi hiyo itakuwa ngumu lakini wachezaji wake wamejipanga kuonyesha kiwango cha juu baada ya kupata mapumziko tofauti na walivyokuwa katika michezo iliyotangulia

Naye Kocha Msaidizi wa Mashujaa, Maulid Makata, amekiri mchezo utakuwa mgumu kwa sababu wanakutana na timu kubwa lakini msimu huu ikiwa bora zaidi kuliko msimu uliopita

Makata amesema hata hivyo wachezaji wake wanapenda kucheza mechi za aina hiyo ambazo zinawatazamaji wengi uwanjani na katika televisheni

"Mechi kama hizi makocha kazi yetu ni kuwajenga tu kisaikolojia kwa sababu wachezaji wenyewe wanazitaka, wanajua zinaonekana na watu wengi kwa hiyo nao wanataka waonekane, wajiuze"

"Tunajua wenzetu ni timu kubwa na wana maandalizi makubwa kuliko sisi, huwezi kutulinganisha na sisi, ukiangalia malengo yao ni kutwaa ubingwa na sisi kubaki Ligi Kuu au nafasi ya nne, ila katika mpira chochote kinaweza kutokea," alisema kocha huyo

More Stories

Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
28m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
22h ago
READ MORE β†’