Transfer - International

Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Novemba 02 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
2 Nov 2024
Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Novemba 02 2024

Meneja wa Manchester United Ruben Amorim anataka kumchukua beki wa kati wa Sporting mwenye umri wa miaka 20 kutoka Ivory Coast Ousmane Diomande, ambaye anakadiriwa na kiwango cha thamani ya pauni milioni 70, kwenda naye Manchester United. (Sun)

Mshambulizi wa Sporting na Uswidi Viktor Gyokeres anaendelea kulengwa na Arsenal na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 sasa anafikiria chaguo lake baada ya kuondoka kwa Amorim - huku kukiwa na uwezekano wa kuhamia London. (TeamTalk)

Manchester United wanaweza kuungana na mahasimu wao wa Primia Ligi Arsenal , Chelsea , Liverpool na Manchester City katika mbio za kumsajili Gyokeres. (Florian Plettenberg, Sky Sports Germany)

Manchester United ni miongoni mwa vilabu vitatu vikubwa barani Ulaya vinavyomfuatilia mshambuliaji wa Real Madrid mwenye umri wa miaka 24 Vinicius Jr, huku ofa ya kandarasi ya euro bilioni moja ikiwa ikijadiliwa. (Relevo, kupitia TeamTalk)

Kiungo wa zamani wa Liverpool na timu ya taifa ya Uingereza Steven Gerrard ameapa kupambana kuendelea kuwa meneja wa Al-Ettifaq baada ya wito wa kumtaka ajiuzulu nafasi hiyo. (Mail)

Kikosi cha kwanza cha Manchester United kinatamani sana meneja wa muda wa Uholanzi Ruud van Nistelrooy aendelee kubakia katika klabu hiyo baada ya Amorim kuchukua mikoba ya Old Trafford. (Sun)

Meneja wa Arsenal Mikel Arteta anataka kumsajili winga wa Bayern Munich wa Ujerumani, Leroy Sane, 28. (Christian Falk, Bild)

The Gunners na klabu nyingine ya Primia Ligi Southampton wana nia ya kumsajili mshambuliaji wa Palmeiras mwenye umri wa miaka 18 Luighi. (Nosso Palmeiras - in Portuguese)

Kocha mkuu wa Chelsea Enzo Maresca anakabiliwa na kizingiti kikubwa iwapo anataka kumchukua beki wa Denmark Patrick Dorgu mwenye umri wa miaka 20 kwenda Stamford Bridge, kwani nyota huyo wa Lecce yuko mbioni kusalia Serie A. (GiveMeSport)

Mkufunzi wa Wolves Gary O'Neil ana michezo miwili pekee kuokoa kibarua chake baada ya kuanza vibaya msimu huu. (Football Insider)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
2h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
3h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
4h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
4h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
5h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
20h ago
READ MORE β†’