Azam Fc imetakata uwanja wa Azam Complex ikiibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Yanga katika mchezo mkali wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa Azam Complex
Azam Fc ilionekana kusaka ushindi mapema kwa kufanya mashambulizi mfululizo katika lango la Yanga
Makosa ya Ibrahim Bacca kumvuta Saadun aliyekuwa anaelekea langoni kuonana na Djigui Diarra yaliigharim Yanga baada ya beki huyo kuonyeshwa kadi nyekundu
Kutolewa kwa Bacca kuliifanya Azam Fc itawale mchezo huo na hatimaye Gibril Sillah akafunga bao dakika chache baadae baada ya kupokea pasi murua kutoka kwa Mtasingwa
Baada ya kufanga bao hilo Wananchi wakazinduka kusaka bao la kusawazisha hata hivyo walishindwa kuipenye ngome ya Azam Fc iliyokuwa ikilindwa na wachezaji 10 nyuma ya mpira
Ni ushindi uliomaliza rekodi ya Yanga kutopoteza mchezo au kuruhusu bao msimu huu
Upande wa Azam Fc ni furaha kwao kwani wameifunga Yanga kwnye ligi 'back 2 back'




