Arsenal bado inamtaka Gyokeres

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd November 2024


Arsenal bado inamtaka Gyokeres

Mshambuliaji wa Sporting Lisbon, Viktor Gyokeres amezidi kuwachanganya mabosi wa Arsenal ambao wanaamini wana nafasi kubwa ya kumsajili baada ya kuondoka kwa kocha Ruben Amorim aliyejiunga na Manchester United

Arsenal ilijaribu kumsajili supastaa huyo katika dirisha lililopita la majira ya kiangazi, lakini ilishindikana na kiliripotiwa kukwamisha dili hilo ni Amorim ambaye alipambana kumshawishi abaki

Staa huyo wa kimataifa wa Sweden katika mkataba wake ana kipengele ambacho kinamruhusu kuondoka ikiwa timu inayomtaka italipa Euro 100 milioni

Timu nyingi barani Ulaya zimevutiwa naye baada ya kiwango bora alichoonyesha tangu msimu uliopita

Katika msimu huu mchezaji huyo amecheza mechi 16 za michuano yote na kufunga mabao 20. Mkataba wake wa sasa unatarajiwa kumalizika ifikapo 2028.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.