Mshambuliaji wa Sporting Lisbon, Viktor Gyokeres amezidi kuwachanganya mabosi wa Arsenal ambao wanaamini wana nafasi kubwa ya kumsajili baada ya kuondoka kwa kocha Ruben Amorim aliyejiunga na Manchester United
Arsenal ilijaribu kumsajili supastaa huyo katika dirisha lililopita la majira ya kiangazi, lakini ilishindikana na kiliripotiwa kukwamisha dili hilo ni Amorim ambaye alipambana kumshawishi abaki
Staa huyo wa kimataifa wa Sweden katika mkataba wake ana kipengele ambacho kinamruhusu kuondoka ikiwa timu inayomtaka italipa Euro 100 milioni
Timu nyingi barani Ulaya zimevutiwa naye baada ya kiwango bora alichoonyesha tangu msimu uliopita
Katika msimu huu mchezaji huyo amecheza mechi 16 za michuano yote na kufunga mabao 20. Mkataba wake wa sasa unatarajiwa kumalizika ifikapo 2028.



