Prisons yaichapa KenGold 1-0

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd November 2024


Prisons yaichapa KenGold 1-0

Bao la mkwaju wa penti dakika ya 53 lililofungwa na Jumanne Elifadhiili limehitimisha mfululizo wa kupoteza mechi kwa Tanzania Prisons wakipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya KenGodl katika mchezo uliopigwa uwanja wa Sokoine

Baada ya kupoteza mechi tatu mfululizo nyumbani, Prisons leo ilikuwa tofauti dhidi ya majirani zao KenGold ambao bado hali yao imeendelea kuwa tete baada ya kipigo hicho

Ushindi huo umeisogeza Tanzania Prisons hadi nafasi ya 12 katika msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 10 huku KenGold wakiendelea kujiweka katika hatari chini kabisa ya msimamo wa ligi

KenGold wamekusanya alama tano tu kutoka mechi 11 walizocheza


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.