Mwishoni mwa wiki klabu ya Yanga kwa kushirikiana na GSM Foundation ilichangia TZS Millioni 50 kwenye harambee maalum iliyoendeshwa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete - JKCI kwa dhumuni la kusaidia matibabu ya watoto 1500 wanaotibiwa kwenye taasisi hiyo
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete - JKCI ilitoa tuzo ya heshima kwa kutambua mchango wa Yanga katika uhamasishaji na uchangiaji fedha wa kusaidia matibabu ya watoto wanaotibiwa katika taasisi hiyo
Tuzo hiyo ilikabidhiwa na Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete na kupokelewa na Mkurugenzi wa Idara ya Masoko na Wanachama wa Yanga, Ibrahim Samwel
