Mshambuliaji wa Pamba Jiji George Mpole amesema licha ya kipindi kigumu ambacho timu hiyo inapitia, watarejea katika ubora na kufanya vizuri katika mechi zilizosalia ligi kuu ya NBC msimu huu
Pamba Jiji inashika nafasi ya 15 katika ligi kuu ya NBC ikikusanya alama 5 kutoka mechi 10
Pamba Jiji ambayo sasa inanolewa na Kocha Freddy Felix Minziro haijashinda mchezo wowote msimu huu
Mpole amesema kama mchezaji anatamani kuona timu hiyo inafanya vizuri, lakini halitawezekana kama hawatapambana katika mechi zilizosalia ili kuhakikisha wanajinusuru kurudi Ligi ya Championship
Mpole amesema jambo muhimu kwao ni kuona wanaanza kushinda mechi na kuongeza morali ya timu
"Tukianza kushinda mechi kujiamini kutaongezeka, morali itakuwa juu, ndio maana tunaendelea kupambana na kuhamasishana hadi tutakapoanza kukaa katika mstari"
"Kwa upande wangu kama mshambuliaji napambana naona ni suala la muda kuanza kuhesabu mabao yangu. Sijawahi kukata tamaa na siyo mtu wa kukata tamaa ninapofanya jambo lolote," alisema Mpole