Mchezo wa Ligi Kuu ya NBC kati ya Simba dhidi ya KMC ambao ulipaswa kupigwa leo katika uwanja wa KMC Complex, ulisogezwa mbele kwa siku moja na sasa utapigwa kesho Jumatano, katika uwanja huo
Bodi ya ligi ilitaja sababu ya mabadiliko hayo ni muingiliano wa ratiba ya mechi za ligi ya Wanawake ambapo leo uwanja wa KMC itachezwa mechi kati ya Yanga Princess dhidi ya Mashujaa Queens
Simba imetangaza viingilio vya mchezo dhidi ya KMC, ambao ni Derby itakayokutanisha timu mbili zinzotumia uwanja wa KMC Complex kama uwanja wao wa nyumbani msimu huu
VIP ni Tsh 20,000/- na Mzunguuko ni Tsh 10,000/-. Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali ametamba kuwa wanakwenda kubeba alama zote tatu mbele ya KMC siku ya Jumatano huku akiwataka mashabiki wa Simba kujitokeza kwa wingi kushuhudia mchezo huo




