AC Milan imepata ushindi wa kihistoria dhidi ya Real Madrid Uwanja wa Santiago Bernabeu katika mechi ya UEFA Champions League Jumanne usiku
The Rossoneri waliwafunga wababe hao wa Uhispania 1-3. Kikosi cha Fonseca kiliibuka kidedea kwa kupata pointi tatu za thamani ugenini kwa mabao ya Malick Thiaw, Alvaro Morata na Tijjani Reijnders.
Morata, mshambuliaji wa zamani wa Real Madrid alisema walihitaji kushinda mchezo huo hivyo walipambana uwanjani mfano wa Simba aliyejeruhiwa
"Niliwaambia wenzangu kabla ya mechi kuwa hii ni mech muhimu haswa kwetu, na kisha kwa mashabiki na kilabu. Ilibidi tupigane kama Simba. Tulicheza mchezo mzuri. Tulikuwa na nyakati bora leo na muhimu kila mmoja alipambana"
"Tunasalia kwenye njia yetu, hakuna haja ya fataki. Ni muhimu kufahamu jinsi kushinda kulivyo muhimu," alisema Morata
Hali inazidi kuwa mbaya kwa Real Madrid ambayo imepoteza mchezo wa pili mfululizo nyumbani huku ikiruhusu mabao 7
Wiki iliyopita Real Madrid walichapwa mabao 4-0 na wapinzani wao wa jadi Fc Barcelona hapo hapo Santiago Bernebeu



