Bodi mpya Singida BS ina vigogo kutoka Simba, Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 6th November 2024


Bodi mpya Singida BS ina vigogo kutoka Simba, Yanga

Vigogo waliowahi kushika nyadhifa mbalimbali kwenye timu za Simba na Yanga kwa nyakati tofauti wametangazwa na Singida Black Stars kuwa katika Bodi ya Wakurugenzi ya klabu hiyo

Viongozi hao waliowahi kuongoza Yanga na sasa wako Singida ni pamoja na Omary Kaya ambaye ameteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi

Kabla ya kujiunga na Singida Black Stars, Kaya alikuwa mtendaji mkuu wa Namungo na aliwahi kukaimu nafasi ya ukatibu mkuu Yanga

Pia yumo Hussein Nyika aliyewahi kuongoza Kamati ya usajili ya Yanga huku mlezi wa Simba Queens Fatema Dewji naye akiwa miongoni mwa Wajumbe wa Bodi

Fatema ni dada yake Rais wa heshima wa klabu ya Simba Mohammed Dewji 'Mo' ambaye pia Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba

Jina la Salah Said Mohammed pia limeorodheshwa katika Wajumbe wa Bodi. salah ni mdogo wa Mdhamini/Mfadhili wa Yanga GSM


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.