Vigogo waliowahi kushika nyadhifa mbalimbali kwenye timu za Simba na Yanga kwa nyakati tofauti wametangazwa na Singida Black Stars kuwa katika Bodi ya Wakurugenzi ya klabu hiyo
Viongozi hao waliowahi kuongoza Yanga na sasa wako Singida ni pamoja na Omary Kaya ambaye ameteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi
Kabla ya kujiunga na Singida Black Stars, Kaya alikuwa mtendaji mkuu wa Namungo na aliwahi kukaimu nafasi ya ukatibu mkuu Yanga
Pia yumo Hussein Nyika aliyewahi kuongoza Kamati ya usajili ya Yanga huku mlezi wa Simba Queens Fatema Dewji naye akiwa miongoni mwa Wajumbe wa Bodi
Fatema ni dada yake Rais wa heshima wa klabu ya Simba Mohammed Dewji 'Mo' ambaye pia Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba
Jina la Salah Said Mohammed pia limeorodheshwa katika Wajumbe wa Bodi. salah ni mdogo wa Mdhamini/Mfadhili wa Yanga GSM




