Baada ya kipigo kutoka kwa Azam Fc, mabingwa watetezi ligi kuu ya NBC Yanga kesho Alhamisi watashuka uwanja wa Azam Complex kumenyana na Tabora katika mwendelezo wa ligi kuu ya NBC
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe ametamba kuwa watakwenda kuikabili Tabora United wakiwa na dhamira moja tu, kurejea katika mwenendo wao wa ushindi
Kamwe amesema anafahamu kupoteza kwa Yanga mchezo uliopita kulipelekea furaha kwa watu wengi ambao hawaitakii mema Yanga, kesho watakwenda kuwapa tabasamu mashabiki wao
"Najua watu wengi ambao hawatutakii mema walifurahi sana baada ya sisi kupoteza dhidi ya Azam Fc. Nawaambia mashabiki wa Yanga waje kwa wingi Azam Complex kesho hii ni siku ya kuirejesha furaha Jangwani," alisema Kamwe
Yanga imetangaza viingilio vya mchezo huo utakaopigwa saa 12 jioni
