Ripoti ya vyombo vya habari vya Uhispania imedai kwamba nyota wa Real Madrid Kylian Mbappe hataki kucheza kama mshambuliaji wa kati katika klabu ya Real Madrid
Kulingana na gazeti la Uhispania la 'Sport', Mbappe amechoshwa kucheza kama mshambuliaji
Chanzo hicho kiliongeza kuwa nyota huyo wa Ufaransa anataka kucheza kama winga wa kushoto badala ya Vinicius Junior
Chanzo hicho kilihitimisha kuwa Mbappe anaamini kushuka kwa kiwango chake kunatokana na kucheza katika nafasi ya mshambuliaji wa moja kwa moja eneo ambalo hakuzoea kucheza kabla
Wakati yuko PSG Mbappe alifunga mabao mengi akitokea pembeni kama winga na amekuwa akifanya hivyo hata anapokuwa na timu ya Taifa ya Ufaransa
Hata hivyo katika klabu ya Real Madrid, kocha Carlo Ancelotti hupendelea kumtumia Vini Jr katika nafasi hiyo kwani amekuwa akifanya vizuri zaidi



