Mbappe hataki kucheza namba 9 Real Madrid

Joel JJ By Joel JJ β€’ 6th November 2024


Mbappe hataki kucheza namba 9 Real Madrid

Ripoti ya vyombo vya habari vya Uhispania imedai kwamba nyota wa Real Madrid Kylian Mbappe hataki kucheza kama mshambuliaji wa kati katika klabu ya Real Madrid

Kulingana na gazeti la Uhispania la 'Sport', Mbappe amechoshwa kucheza kama mshambuliaji

Chanzo hicho kiliongeza kuwa nyota huyo wa Ufaransa anataka kucheza kama winga wa kushoto badala ya Vinicius Junior

Chanzo hicho kilihitimisha kuwa Mbappe anaamini kushuka kwa kiwango chake kunatokana na kucheza katika nafasi ya mshambuliaji wa moja kwa moja eneo ambalo hakuzoea kucheza kabla

Wakati yuko PSG Mbappe alifunga mabao mengi akitokea pembeni kama winga na amekuwa akifanya hivyo hata anapokuwa na timu ya Taifa ya Ufaransa

Hata hivyo katika klabu ya Real Madrid, kocha Carlo Ancelotti hupendelea kumtumia Vini Jr katika nafasi hiyo kwani amekuwa akifanya vizuri zaidi


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.