Simba yaifumua KMC mabao 4-0

Joel JJ By Joel JJ β€’ 6th November 2024


Simba yaifumua KMC mabao 4-0

Simba imeendelea kudhihirisha kuwa inautaka ubingwa wa ligi kuu msimu huu wakiichapa KMC mabao 4-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa KMC Complex

Simba ilitawala mchezo huo na pengine mambo yangekuwa mabaya zaidi kwa KMC kama washambuliaji wa Simba wangekuwa makini

Awesu Awesu ndiye aliyefungua kalamu ya mabao kwa upande wa Simba akiwaadhibu waajiri wake hao wa zamani

Mabao mengine yalifungwa Jean Charles Ahoua aliyepachika mabao mawili na Edwin Balua

Ahoua sasa amefikisha mabao matano akiwa nyuma wa kinara wa mabao Suleiman Mwalimu kwa tofauti ya bao moja tu

Ahoua amehusika katika mabao 9 ya Simba msimu huu pia akitoka pasi 4 za mabao

Simba imepanda kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 25 na kuishusha Yanga yenye alama 24 katika nafasi ya pili


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.