Local,Normal News,Yanga, Tabora

Bacca, Job kuikosa Tabora United

Joel JJ By Joel JJ
β€’
7 Nov 2024
Bacca, Job kuikosa Tabora United

Mabingwa watetezi Ligi Kuu ya NBC Yanga leo wako dimbani Azam Complex kuikabili Tabora United katika mchezo utakaopigwa saa 12 jioni

Yanga inakwenda katika mchezo huo bila ya walinzi wake tegemeo Ibrahim Bacca na Dickson Job wanaotumikia adhabu

Bacca alionyeshwa kadi nyekundu katika mchezo dhidi ya Azam Fc ambapo atakosa mechi tatu huku Job akitumikia adhabu ya kadi tatu za njano

Yanga pia huenda wakakosa huduma ya mlinzi wa kulia Yao Kouassi, mkufunzi wa Yanga Miguel Gamondi akithibitisha bado hajapona majeraha aliyopata katika mchezo dhidi ya Coastal Union

Ni mchezo unaotarajiwa kuwa na upinzani mkali, Tabora United wako katika kiwango bora wakishinda mechi mbili zilizopita dhidi ya Mashujaa na Pamba Jiji

Aidha huenda leo nyota wa zamani wa Yanga, washambuliaji Heritier Makambo na Yacouba Songne wakaongoza safu ya ushambuliaji ya Tabora United dhidi ya waajiri zao hao wa zamani

Yanga wako nafasi ya pili katika msimamo wa ligi wakiwa na alama 24, nyuma ya watani zao Simba wanaoongoza ligi baada ya ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya KMC jana na kufikisha alama 25

Kama Yanga itaibuka na ushindi leo basi itarejea juu ya msimamo huku Tabora United wakiwa nafasi ya sita na alama 14

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’