Local,Normal News,Prisons, JKT

Prisons kuweka kambi Dar

Joel JJ By Joel JJ
β€’
8 Nov 2024
Prisons kuweka kambi Dar

Klabu ya Prisons imesema mapumziko ya Kalenda ya Kimataifa kuweka kambi yake jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujiandaa na michezo ijayo ya Ligi Kuu Tanzania Bara, imeelezwa.

Ligi Kuu Tanzania Bara imesimama kupisha michezo ya kimataifa, huku wachezaji wengi wakitimkia katika vikosi vya timu zao za taifa vinavyosaka tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON), zitakazofanyika mwakani nchini, Morocco

Mtendaji Mkuu wa Prisons, John Matei, amesema kikosi cha timu hiyo kitaanza mazoezi yake rasmi kesho baada ya wachezaji kumaliza mapumziko ya siku sita

Matei alisema baada ya kuifunga KenGold bao 1-0 Jumapili iliyopita, waliamua kuwapa wachezaji wao mapumziko mafupi kwa sababu mechi yao inayofuata dhidi ya JKT Tanzania itachezwa Novemba 24, mwaka huu

"Baada ya kumaliza mechi ya KenGold tulivunja kambi na kuwapa vijana mapumziko ya kama wiki moja au siku sita hivi, Novemba 9 wanatakiwa kurejea kambini kujiandaa na michezo ijayo, kambi yetu kama kila kitu kikienda sawa, tutayafanyia Dar es Salaam, na kipindi chote hiki cha mapumziko ya FIFA, sisi tutakuwa kambini," Matei alisema

Matei alisema sababu kubwa ya kuweka kambi Dar es Salaam ni kuwa karibu na eneo ambalo mchezo wao dhidi ya JKT Tanzania utachezwa

"Mchezo wetu wa kwanza baada ya mapumziko hayo ni dhidi ya JKT Tanzania uatakaochezwa Dar es Salaam, na hiyo ndiyo sababu kubwa imesababisha tuwe huko karibu zaidi au sehemu hiyo hiyo ambayo tutacheza mchezo wetu wa Novemba 24," Matei aliongeza

Prisons iliyoko chini ya Kocha Mkuu, Mbwana Makata, ipo katika nafasi ya 12 kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara ikiwa na pointi 10 kibindoni baada ya kucheza michezo 10, imeshinda miwili, sare nne na kupoteza mechi nne

Kikosi cha JKT Tanzania nacho kinaendelea na mazoezi huku uongozi ukisema wachezaji wote walioumia katika ajali wanaendelea vyema na wameanza mazoezi mepesi chini ya uangalizi wa madaktari wa timu hiyo

IPP Media

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
4h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
7h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
9h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
11h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
13h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
14h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
14h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
16h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
19h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’