Kwa sasa furaha imetawala Msimbazi baada ya Simba kujichimbia kileleni mwa msimamo wa ligi jana wakijihakikishia kubaki hapo kwa muda mrefu baada ya watani zao Yanga kuangukia pua mbele ya Tabora United wakichapwa mabao 3-1
Matokeo hayo yaliiacha Yanga katika nafasi ya pili ikiwa na alama 24 huku Simba ikibaki kileleni na alama 25 kila timu ikiwa imecheza mechi 10
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali ametamba kuwa msimu huu hakuna wa kuwazuia kutwaa ubingwa wa ligi kuu
Aidha Ahmed amewatahadharisha watani zake Yanga kuwa kama wanataka kuhama dimba la Azam Complex, wasifikirie kabisa kuhamia uwanja wa KMC kwani huko watashuka daraja kabisa
"Nimesikia baada ya kupoteza mechi mbili Azam Complex wanataka kuhama uwanja. Niwatahadharishe wasifikirie kuhamia KMC Complex kwani hii ni himaya yetu sasa"
"Kama wanataka mechi zao zionekane TV 3 basi waje hapa KMC Complex, watacheza ligi ya Championship msimu ujao," alitamba Ahmed
Kumekuwa na tetesi kuwa Yanga inaweza kuhama uwanja wa Azam Complex zikiibuka tuhuma kuwa wanahujumiwa na wamiliki wa uwanja huo Azam Fc



