Local,Normal News,Azam

Bajana apania kurudi kikosi cha kwanza Azam Fc

Joel JJ By Joel JJ
β€’
9 Nov 2024
Bajana apania kurudi kikosi cha kwanza Azam Fc

Baada ya kuwa nje ya uwanja wa takribani mwaka mzima, kiungo wa Azam Fc Sospeter Bajana amesema ana kazi ya kufanya ili kuhakikisha anarejea katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo

Eneo la kiungo la Azam Fc inayoshika nafasi ya nne katika msimamo wa ligi kwa sasa linamilikiwa na viungo James Akaminko na Adolf Mtasingwa huku Feisal Salum 'Fe Toto' akitumika kama kiungo mshambuliaji

Bajana amekiri sio rahisi kurudi moja kwa moja kikosini kutokana na uwepo wa wachezaji hao ambao wanafanya vizuri hivyo analazimika kupambana katika uwanja wa mazoezi

"Nilikuwa nje ya uwanja ni mwaka sasa siwezi nikarwejea moja kwa moja kucheza wakati kuna wachezaji wanafanya vizuri na wanaipambania timu kufikia malengo nina kazi ya kufanya kuhakikisha namshawishi kocha aniamini na kunipa nafasi"

"Naheshimu ubora wa Adolf Mtasingwa na James Akaminko ambao wamekuwa wakicheza nafasi ambayo na mimi naicheza kila mmoja anafanya majukumu yake kwa ubora nafikiri ili kuweza kucheza natakiwa kufanya kazi ya ziada" alisema

Kocha wa Azam Fc Rachid Taoussi amesema wachezaji wengi eneo moja na wote wakiwa bora ni chachu ya mafanikio kwake kutokana na wingi wa mechi na ratiba ngumu ya mechi mfululizo itamsaidia kufanya mabadiliko ya mara kwa mara

"Kuna mechi nyingi nafurahia wachezaji wengi wamerudi na wengine wanarudi kidogo kidogo naamini wote wakiwa kwenye ubora unaotakiwa tutakuwa na timu ambayo inaonyesha ushindani kwa wapinzani bila kuchoka kutokana na mabadiliko ya mara kwa mara eneo hilo la kiungo"

"Bajana bado hajawa fiti lakini tayari ameanza mazoezi ni mchezaji mzuri ataongeza kitu hasa ushindani katika eneo la kiungo mkabaji ambalo tayari wachezaji waliopo wameonyesha uwezo mkubwa," alisema

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’