Frank Lampard anaongoza orodha ya wakufunzi wanaowana majukumu ya kuwa meneja wa kudumu wa Coventry City, mtandao wa talkSPORT umeripoti
Sky Blues ilimtimua kocha wake wa muda mrefu Mark Robins wiki hii baada ya kuanza kwa msimu vibaya na kuiacha klabu hiyo ikiwa nafasi ya 17 kwenye michuano hiyo
Kiungo huyo wa zamani wa England Lampard ndiye anayepewa nafasi kubwa ya kuchukua hatamu kwenye Uwanja wa CBS Arena
Lampard amekuwa nje ya kazi tangu alipomaliza muda wake kama meneja wa muda wa Chelsea mwaka 2023
Alikuwa amechukua usukani Stamford Bridge kwa mara ya pili baada ya kutimuliwa kwa Graham Potter. Jukumu la mwisho la Lampard lilikuwa na Everton