Gamondi aibuka mazoezi ya Yanga Gymkhana

Joel JJ By Joel JJ β€’ 11th November 2024


Gamondi aibuka mazoezi ya Yanga Gymkhana

Baada ya kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Tabora United, tetesi ziligubika hatma ya Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi

Uongozi wa mabingwa hao wa soka Tanzania Bara kwa misimu mitatu mfululizo ulitaka majibu kutoka kwake kwa nini timu imepoteza mechi mbili mfululizo?

Hata hivyo inaonekana Gamondi amepewa nafasi nyingine baada ya leo kuonekana akisimamia mazoezi yaliyofanyika katika Gymkhana

Yanga imerejea mazoezini leo baada ya mapumziko ya siku chache kuanza maandalizi ya mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Al Hilal utakaopigwa Novemba 26 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga, Alex Ngai, amesema bado wana imani na Gamondi akiwataka wanachama na mashabiki wa timu hiyo kutokuwa na wasiwasi wowote kwani viongozi wa Yanga bado wana ushirikiano na kocha huyo pamoja na benchi lake la ufundi


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.