International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne Novemba 12 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
12 Nov 2024
Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne Novemba 12 2024

Arsenal wako tayari kutumia pauni milioni 83 (euro milioni 100) kumnunua kiungo wa kati wa West Ham Mohammed Kudus huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Ghana mwenye umri wa miaka 24 akitaka kujiunga na The Gunners kucheza soka la Ulaya. (Fichajes - In Spanish)

Tottenham wako tayari kukataa nia mpya ya Real Madrid ya kumnunua beki wa Argentina, Cristian Romero, 26. (Football Insider)

Manchester United wanafikiria kumtoa mshambuliaji wa Uholanzi Joshua Zirkzee mwenye umri wa miaka 23 mwezi Januari huku klabu za Serie A zikimfuatilia. (Calciomercato - In Italy)

Juventus wako mstari wa mbele katika vita vya kumsajili mshambuliaji wa Canada Jonathan David, 24, kutoka Lille huku Manchester United, Liverpool na Inter Milan pia zikimuwania. (Footmercato – In french)

Manchester City wameelekeza macho yao kwa mlinda lango wa AC Milan na Ufaransa Mike Maignan, 29. Borussia Dortmund wanafikiria kumnunua kiungo wa kati wa Sunderland mwenye umri wa miaka 19 Jobe Bellingham Januari. (Alan Nixon via Newcastle Chronicle)

Beki wa Bayern Munich Alphonso Davies yuko tayari kuungana tena na mkufunzi wa zamani Hansi Flick katika klabu ya Barcelona licha ya kutaka kumnunua mchezaji huyo wa kimataifa wa Canada mwenye umri wa miaka 24 kutoka Real Madrid na Manchester United. (Team Talks)

Kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba, 31, anakaribia kufikia makubaliano ya kusitisha mkataba wake na Juventus na kusaini klabu nyingine kama mchezaji huru pindi marufuku yake itakapokamilika. (Sky Sports)

Winga wa Ujerumani Leroy Sane ana nia ya kusaini kandarasi mpya katika klabu ya Bayern Munich lakini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 bado yuko njia mojawapo ya kufikia makubaliano kuhusu mkataba. (Florian Plettenberg)

Beki wa zamani wa Uhispania Sergio Ramos, 38, hatarejea Real Madrid lakini watasajili beki wa kati mwezi Januari, huku beki wa Bayer Leverkusen ya Ujerumani Jonathan Tah, 28, akiibuka kama mgombea mpya. (Diario AS – In Spanish)

Skauti kutoka ndani na nje ya nchi wanafuatilia maendeleo ya Kiano Dyer katika klabu ya Chelsea huku kiungo huyo wa kati wa Muingereza, 17, akikaribia mwaka wa mwisho wa kandarasi yake ya sasa. (Mail)

Uingereza iko tayari kufanya mazungumzo zaidi wakati wa mapumziko ya kimataifa juu ya kujaribu kuongeza kocha wa makipa wa Chelsea Henrique Hilario kwenye ofisi ya mkufunzi mkuu anayekuja Thomas Tuchel. (Telegraph – Subscription required)

David Moyes anatazamia kurejea katika usimamizi wa ligi ya Premier huku Crystal Palace, Wolves, Southampton na Leicester zikimtaka. (Sportsport)

Frank Lampard ni mgombea wa nafasi ya meneja iliyoachwa wazi katika klabu ya Championship Coventry City. (Sky Sports)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
2h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
3h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
4h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
4h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
5h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
20h ago
READ MORE β†’