Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa klabu ya KMC FC, Songoro Mnyonge, amesema Kocha wao Mkuu Abdihamid Moallin ameondoka kunako klabu hiyo kwenda kujiunga na klabu ya Yanga
Songoro amesema Moallin alikuwa na mkataba wa mwaka mmoja kuitumikia KMC hivyo wao wanalaani kitendo hicho cha utoro alichofanya
"Ni kweli kocha wetu Moallin ametoroka kazini. Taarifa ya kuondoka kwake tuliipata kutoka kwa wachezaji baada ya mazoezi jana jioni"
"Tulimtafuta mara kadhaa bila mafanikio lakini baadae alipatikana na kuthibitisha ameondoka KMC"
"Sisi tunalaani kitendo hicho kwani ni kinyume na ustaarabu. Yanga wanafahamu Moallin ni kocha wetu walipaswa kututaarifu mapema kumuhitaji kocha wetu kwani bado ana mkataba nasi," alisema Songoro
Awali kocha huyo alikuwa akihusishwa kutimkia Afrika Kusini lakini sasa imethibitishwa Moallin ni Mwananchi