Local,Normal News,Yanga, Simba, Azam, Fountain Gate, Singida BS

Stars kuifuata Ethiopia Alhamisi

Joel JJ By Joel JJ
β€’
13 Nov 2024
Stars kuifuata Ethiopia Alhamisi

Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, inatarajia kuondoka nchini kesho Alhamisi kwa ajili ya mchezo wa tano wa kusaka tiketi ya kufuzu ushiriki wa fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025, dhidi ya Ethiopia, mechi itakayopigwa Jumamosi

Stars inaingia katika mchezo huo wa tano wa kundi 'H' ikiwa na kumbukumbu ya kulazimishwa suluhu mechi ya mwisho dhidi ya Ethiopia iliyopigwa Septemba 4, mwaka huu, huku kwa upande wa Wahabeshi hao wakipoteza kwa mabao 3-0, mbele ya Guinea

Akizungumzia maandalizi kwa ujumla, kaimu kocha mkuu wa Stars, Hemed Suleimani 'Morocco' alisema, licha ya ugumu wa mchezo huo ila wao kama benchi la ufundi na wachezaji kiujumla wamejipanga kuhakikisha wanapata matokeo chanya ugenini

"Kila mmoja wetu yupo tayari kwa changamoto nyingine, tunatambua wapinzani wetu wamekuwa na matokeo yasiyoridhisha sana ila tutacheza kwa tahadhari ya kuhakikisha tunashinda, mchezo huu utatoa taswira yetu ya kufuzu AFCON mwakani Morocco"

"Wenzetu DR Congo walishafuzu hivyo presha ipo kwetu na Guinea ambayo iko juu yetu kwenye msimamo, mchezo na Ethiopia tunauangalia kwa jicho la tatu kwa sababu ndio utakaotupa matumaini makubwa kuelekea mechi ya mwisho hapa Dar es Salaam,"  alisema Morocco

Stars itacheza mchezo huo utakaopigwa kuanzia saa 1:00 usiku kwenye Uwanja wa des Martyrs huko Congo na baada ya hapo itacheza na Guinea jijini Dar es Salaam Novemba 19

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’