International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi Novemba 14 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
14 Nov 2024
Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi Novemba 14 2024

Manchester United na Arsenal wanapigania kumsajili winga wa zamani wa Manchester City Leroy Sane kutoka Bayern Munich, huku mkataba wake wa kimataifa wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 28 ukimalizika msimu ujao. (Bild - In Germany subscription required)

Liverpool ipo katika mazungumzo na mshambuliaji wa Misri mwenye umri wa miaka 32 Mohamed Salah kuhusu uwezekano wa kumpa kandarasi mpya lakini pande hizo kwa sasa hazijaafikia makubaliano yoyote. (Florian Plettenberg)

Arsenal wanafuatilia hali ya kiungo wa kati wa Real Sociedad na Uhispania Martin Zubimendi, kwa kuamini wanaweza kuthibitisha kuwa mahali pazuri zaidi kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25. (Independent) Barcelona na Real Madrid wanamfuatilia beki wa kati wa Nottingham Forest raia wa Brazil Murillo, 22. (Sport in Spanish)

Manchester United wanamtaka beki wa kushoto wa Bournemouth na Hungary Milos Kerkez, 21. (Football Transfers)

Liverpool wanafikiria kumnunua mshambuliaji wa PSV Eindhoven, Ricardo Pepi, na mchezaji huyo wa kimataifa wa Marekani mwenye umri wa miaka 21 pia yupo kwenye rada za Bayern Munich, Borussia Dortmund na Atletico Madrid. (Caughtoffside)

Manchester United wanafikiria uhamisho wa Januari kumnunua kiungo wa kati wa Dinamo Zagreb na Croatia Martin Baturina, 21, ambaye pia amekuwa akitazamwa na Barcelona na Atletico. (Teamtalks)

West Ham wanamtazama fowadi wa Botafogo na Brazil Igor Jesus, 23, kama chaguo la kuimarisha safu yao ya ushambuliaji. (Football Insider)

Wakuu wa Newcastle United bado wametulia kuhusu hali ya kandarasi ya mshambuliaji wa Uswidi Alexander Isak, licha ya madai mapya kwamba mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 hajatulia katika klabu hiyo. (Newcastle Chronicle)

Tottenham wametoa kiasi kikubwa cha pesa kumnunua beki mpya wa kati katika dirisha la uhamisho la Januari. (Football Insider)

Mkurugenzi wa michezo wa Real Sociedad Roberto Olabe ataondoka katika klabu hiyo ya La Liga mwishoni mwa msimu huu na kuzingatiwa nafasi hiyo katika klabu ya Arsenal, iliyoachwa wazi na Edu hivi majuzi. (Times – Subscription)

Tottenham wameanza mchakato wa kuamsha kipengele cha kuongeza mkataba wa mshambuliaji Son Heung-min, 32, hadi Juni 2026. (Fabrizio Romano)

Beki wa zamani wa Real Madrid na Uhispania Sergio Ramos, 38, yuko kwenye mazungumzo ya hali ya juu na klabu ya Brazil ya Corinthians na hatarejea Bernabeu, licha ya tatizo la majeruhi la klabu hiyo ya La Liga. (Sport - Spanish)

Kipa wa Newcastle Odysseas Vlachodimos, 30, anataka kusalia na kupigania nafasi yake St James' Park ingawa Magpies wanatazamia kumleta James Trafford mwenye umri wa miaka 22 kutoka Burnley msimu ujao wa joto. (Subscription Required)

Chelsea imewaweka beki wa Benfica Mreno Tomas Araujo na mlinzi wa kati wa Bournemouth Illia Zabarnyi, 22, wa Benfica, 22, kwenye orodha ya wachezaji wanaotarajiwa kuwalinda. (Football Transfer)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’