Shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA limepanga kuanzisha mfumo mpya wa Football Video Support utakaoitwa kwa kiufupi Kwa jina la FVS
Mfumo huo unaandaliwa Ili kuja kuwa mbadala wa Video Assistant Referee VAR
FIFA wameeleza kuwa mfumo huo utakuwa Bora zaidi na rahisi kutumika
FVS utakuwa na camera system kuanzia 4-5 kwa ajili ya kufanya review ya matukio tata yanayotakiwa kufanyiwa maamuzi sahihi
Makocha wa timu mbili zitakazokuwa kiwanjani wanaruhusiwa kumwambia mwamuzi akafanye review mara mbili ndani ya mchezo kama kuna matukio wameona hajatoa maamuzi sahihi
Mwamuzi pekee ndie atakaeruhusiwa kwenda kuangalia review kwenye FVS pindi atakapopokea malalamiko ya makocha kwenye matukio tata ambayo maamuzi yake wanaona kama hayajaenda sawa



