Klabu ya Coastal Union imewatangazia wanachama wake kuwa itafanya uchaguzi mkuu wa viongozi wa klabu hiyo kwa mujibu wa katiba ambayo inawataka kuchagua viongozi wapya kila baada ya miaka 4
Uchaguzi huo utahusisha nafasi ya Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti pamoja na wajumbe wa kamati ya utendaji
Taratibu za zoezi hilo zinaanza hapo kesho tarehe 15/11/2024 na hatua ya uchukuaji fomu na baadae kutakuwa na zoezi la kujadiliwa wagombea, kuchujwa kwa wagombea, rufaa za wagombea na hatimae siku ya wajumbe wa mkutano mkuu kupiga kura siku ya tarehe 16/12/2024




