Beki wa kulia wa Liverpool Trent Alexander-Arnold anaendelea kukataa ofa za kuongeza mkataba wake Anfield huku Real Madrid wakiendelea na mazungumzo ya kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 mkataba wake wa sasa utakapokamilika msimu ujao wa joto. (Relevo - Spanish)
West Ham wanatarajiwa kusimama kidete kumuuza kiungo mshambuliaji wa Ghana Mohammed Kudus kwa pauni milioni 85 huku Arsenal na Liverpool zikimfuatilia mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24. (Mail – Subscription Required)
Kocha wa Bayer Leverkusen Xabi Alonso ataondoka katika klabu hiyo ya Bundesliga mwishoni mwa msimu huu licha ya kusaini kandarasi hadi 2026, huku Real Madrid ikitarajiwa kuwa eneo analotarajiwa kuelekea. (Eurosport In Spanish)
Barcelona wanavutiwa na beki wa kushoto wa Wolves Mhispania Hugo Bueno, 22, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo katika klabu ya Feyenoord ya Uholanzi. (Sport – In Spanish)
Real Madrid wamefanya uchunguzi wa kwanza kutaka kumsajili beki wa kati wa kimataifa wa Ujerumani wa Bayer Leverkusen Jonathan Tah. Barcelona, Bayern Munich na vilabu vya Premier League vinadaiwa kumfuatilia beki huyo ambaye mkataba wake na Leverkusen unamalizika mwishoni mwa msimu huu. (AS – In Spanish)
BBC



