Singida Black Stars yashusha mshambuliaji Mghana

Joel JJ By Joel JJ β€’ 15th November 2024


Singida Black Stars yashusha mshambuliaji Mghana

Klabu ya Singida Black Stars inatajwa kukamilisha usajili wa mshambuliaji Jonathan Sowah raia wa Ghana

Sowah ataanza kuitumikia Singida BS mwezi ujao pale dirisha dogo la usajili litakapofunguliwa

Chanzo kutoka ndani ya uongozi wa Singida BS, kimethibitisha kuwa mshambuliaji huyo aliyekuwa akiitumikia Al Nasr Benghazi ya Libya, tayari yuko nchini

Katika dirisha lililopita la usajili, Sowah alihusishwa kujiunga na Yanga lakini Benghazi hawakuwa tayari kumuuza kwa wakati huo

Kabla ya kuelekea Libya, Sowah (25) aliitumikia Medeama Fc ambapo msimu uliopita ilikuwa kundi moja na Yanga katika michuano ya ligi ya mabingwa hatua ya makundi


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.