Klabu ya Singida Black Stars inatajwa kukamilisha usajili wa mshambuliaji Jonathan Sowah raia wa Ghana
Sowah ataanza kuitumikia Singida BS mwezi ujao pale dirisha dogo la usajili litakapofunguliwa
Chanzo kutoka ndani ya uongozi wa Singida BS, kimethibitisha kuwa mshambuliaji huyo aliyekuwa akiitumikia Al Nasr Benghazi ya Libya, tayari yuko nchini
Katika dirisha lililopita la usajili, Sowah alihusishwa kujiunga na Yanga lakini Benghazi hawakuwa tayari kumuuza kwa wakati huo
Kabla ya kuelekea Libya, Sowah (25) aliitumikia Medeama Fc ambapo msimu uliopita ilikuwa kundi moja na Yanga katika michuano ya ligi ya mabingwa hatua ya makundi



