Gamondi afutwa kazi Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 15th November 2024


Gamondi afutwa kazi Yanga

Zilianza kama tetesi hatimaye leo uongozi wa Yanga umetangaza kuachana na aliyekuwa kocha wake mkuu Miguel Gamondi pamoja na Kocha Msaidizi Moussa Ndaw

Kupitia taarifa rasmi iliyotolewa na Yanga mapema leo, mikataba ya makocha hao imesitishwa mara moja huku mchakato wa kusaka warithi wao ikianza

Kibarua cha Gamondi kiliingia mashakani baada ya kupoteza mechi mbili za ligi kuu dhidi ya Azam Fc na Tabora United

Aliyekuwa Kocha wa KMC Abdihamid Moallin anatarajiwa kutangazwa kuwa kocha msaidizi wa Yanga huku Kheireddine Madoui raia wa Algeria akitarajiwa kuwa kocha mkuu akitokea klabu ya CS COnstantine


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.