Yanga imekuja na surprise ya aina yake baada ya kumtangaza Sead Ramovic kuwa Kocha Mkuu akichukua nafasi iliyoachwa na Miguel Gamondi
Awali jina la kocha raia wa Algeria Kheireddine Madoui ndio lililokuwa likitajwa zaidi kumrithi Gamondi
Ramovic ni kocha raia wa Ujerumani ambaye alikuwa akiinoa klabu ya TS Galaxy inayoshiriki ligi kuu ya Afrika Kusini
Kabla ya Galaxy aliwahi kuwa kocha msaidizi wa Novi Pazar iliyopo ligi kuu nchini Serbia
Ramovic (45) si kocha mwenye CV kubwa sana lakini kama mchezaji ametamba katika klabu mbalimbali kunako ligi kuu ya Ujerumani, Bundesliga
Yanga inakuwa klabu yake ya pili kuifundisha Afrika baada ya TS Galaxy



