Sead Ramovic arithi mikoba ya Gamondi Yanga

Joel JJ By Joel JJ • 15th November 2024


Sead Ramovic arithi mikoba ya Gamondi Yanga

Yanga imekuja na surprise ya aina yake baada ya kumtangaza Sead Ramovic kuwa Kocha Mkuu akichukua nafasi iliyoachwa na Miguel Gamondi

Awali jina la kocha raia wa Algeria Kheireddine Madoui ndio lililokuwa likitajwa zaidi kumrithi Gamondi

Ramovic ni kocha raia wa Ujerumani ambaye alikuwa akiinoa klabu ya TS Galaxy inayoshiriki ligi kuu ya Afrika Kusini

Kabla ya Galaxy aliwahi kuwa kocha msaidizi wa Novi Pazar iliyopo ligi kuu nchini Serbia

Ramovic (45) si kocha mwenye CV kubwa sana lakini kama mchezaji ametamba katika klabu mbalimbali kunako ligi kuu ya Ujerumani, Bundesliga 

Yanga inakuwa klabu yake ya pili kuifundisha Afrika baada ya TS Galaxy


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.