International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Novemba 16 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
16 Nov 2024
Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Novemba 16 2024

Pep Guardiola, 53, amefikia makubaliano ya kimsingi ya kuongezwa kwa mwaka mmoja mkataba wake Manchester City. (Football Insider)

Manchester United itakabiliana na ushindani kutoka kwa Union Berlin kumsajili kiungo wa kati wa Ujerumani Leon Goretzka, 29, ambaye anatatizika na hali yake katika klabu ya Bayern Munich. (Team Talk)

Ruud van Nistelrooy ametuma ombi la kuwa kocha mkuu wa Coventry City baada ya kuacha nafasi yake kama kocha msaidizi wa Manchester United. (Talksport)

Fulham wameungana na wapinzani wao wa London Brentford kumwinda mshambuliaji wa Botafogo na Brazil Igor Jesus, 23. Newcastle United na Nottingham Forest pia wanavutiwa na mchezaji huyo. (TBR)

Juventus wanakamia kumnunua beki wa Fulham na Denmark Joachim Andersen, 28, na mlinzi wa Chelsea na Ufaransa Benoit Badiashile, 23. (La Gazzetta dello Sport)

West Ham wanamfuatilia kwa karibu beki wa Brighton Tariq Lamptey, 24, na wako katika nafasi nzuri ya kushinda Everton katika mbio za kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Ghana msimu ujao kwa uhamisho wa bure. (Football Insider)

Tottenham pia wanataka kumnunua Lamptey kwa nia ya kuimarisha safu ya ulinzi ya Ange Postecoglou wakati wa uhamisho wa wacheziji wa Januari. (Teamtalk)

Barcelona wanavutiwa na winga wa Napoli na Georgia Khvicha Kvaratskhelia. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 anakadiriwa kuwa na thamani ya euro milioni 67. (Repubblica, kwa Kiitaliano - usajili unahitajika)

Beki wa Ujerumani Mats Hummels, 35, huenda akaamua kustaafu ikiwa hatapata nafasi ya kuondoka Roma mwezi Januari. (Sky, kwa Kijerumani)

Manchester United wanaamini kuwa huenda wakahitaji kufanya uamuzi wa kumnunua mchezaji wa Rosenborg Sverre Nypan,17, haraka iwezekanavyo ili wapate saini ya kiungo huyo wa kati wa Norway. (Givemesport)

Bayern Munich wanafikiria kumsajili mshambuliaji wa Lille na Canada Jonathan David. Mkataba wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 unamalizika msimu ujao na hana mpango wa kusaini mkataba mpya. (Anga, kwa Kijerumani)

Beki wa Bayern Munich na Canada Alphonso Davies, 24, anajua Real Madrid wako tayari kukubali masharti yake na makubaliano ya awali ya kandarasi yanasubiriwa tarehe 2 Januari. (Marca)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
2h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
3h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
4h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
4h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
5h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
20h ago
READ MORE β†’