Kuzishuhudia Yanga, Al Hilal kiingilio 3,000

Joel JJ By Joel JJ β€’ 16th November 2024


Kuzishuhudia Yanga, Al Hilal kiingilio 3,000

Mapema leo Yanga ilitangaza viingilio vya mchezo wa kwanza hatua ya makundi michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Al Hilal utakaopigwa Jumanne, Novemba 26 katika uwanja wa Benjamin Mkapa, saa 10 jioni

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe alitaja viingilio hivyo ambapo VIP A ni Tsh 30,000/-, VIP B Tsh 20,000/-, VIP C Tsh 10,000/-, Machungwa na Mzunguuko ni Tsh 3,000/-. Kamwe alisema mauzo ya tiketi yameanza leo kupitia mitandao ya simu

Msemaji huyo wa Yanga amewataka mashabiki na wanachama wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi uwanja wa Benjamin Mkapa ili kuipa hamasa timu yao

Kamwe amesema haijawahi kutokea Yanga ikapoteza mechi tatu mfululizo katika mashindano tofauti hivyo hawako tayari kuona wanakosa ushindi katika mchezo dhidi ya Al Hilal

Kuzindua jezi Novemba 20

Katika hatua nyingine, Kamwe amesema Yanga inatarajiwa kuzindua jezi za Ligi ya Mabingwa, Novemba 20, Makao Makuu ya klabu hiyo, Jangwani

Kamwe amesema jezi zitaanza kupatikana Makao Makuu ya klabu na maduka ya GSM kwa Tsh 50,000/-


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.