Mapema leo Yanga ilitangaza viingilio vya mchezo wa kwanza hatua ya makundi michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Al Hilal utakaopigwa Jumanne, Novemba 26 katika uwanja wa Benjamin Mkapa, saa 10 jioni
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe alitaja viingilio hivyo ambapo VIP A ni Tsh 30,000/-, VIP B Tsh 20,000/-, VIP C Tsh 10,000/-, Machungwa na Mzunguuko ni Tsh 3,000/-. Kamwe alisema mauzo ya tiketi yameanza leo kupitia mitandao ya simu
Msemaji huyo wa Yanga amewataka mashabiki na wanachama wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi uwanja wa Benjamin Mkapa ili kuipa hamasa timu yao
Kamwe amesema haijawahi kutokea Yanga ikapoteza mechi tatu mfululizo katika mashindano tofauti hivyo hawako tayari kuona wanakosa ushindi katika mchezo dhidi ya Al Hilal
Kuzindua jezi Novemba 20
Katika hatua nyingine, Kamwe amesema Yanga inatarajiwa kuzindua jezi za Ligi ya Mabingwa, Novemba 20, Makao Makuu ya klabu hiyo, Jangwani
Kamwe amesema jezi zitaanza kupatikana Makao Makuu ya klabu na maduka ya GSM kwa Tsh 50,000/-



