Local,Normal News,Pamba, Simba

Pamba Jiji mguu sawa kuikabili Simba

Joel JJ By Joel JJ
β€’
16 Nov 2024
Pamba Jiji mguu sawa kuikabili Simba

Pamba Jiji Fc imetamba kuwa kuwa klabu ya Simba isitarajie mteremko katika mechi itakayowakutanisha ya Ligi Kuu Tanzania Bara itakayochezwa Novemba 22, mwaka huu kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini, Mwanza

Kocha Msaidizi wa timu hiyo, Mathias Wandiba, amesema Simba anakwenda Mwanza katika wakati mbaya kwa sababu malengo yao ni kushinda mechi nne zilizobaki za mzunguko wa kwanza

Wandiba amesema Pamba Jiji inawaambia Simba wajiandae kukutana na ushindani kutokana na wao kuhitaji ushindi katika mechi zote zilizobakia za mzunguko wa kwanza ambazo watacheza nyumbani

"Dhamira yetu ni kufanya vizuri katika michezo yetu minne iliyobaki ya mzunguko wa kwanza, michezo miwili tutacheza nyumbani dhidi ya Simba, Ijumaa ijayo na KenGold, Desemba Mosi, hii tumejiwekea mikakati ni lazima tushinde"

"Kwa bahati nzuri moja kati ya michezo hii mwili tunacheza na Simba, wamekuja kwenye wakati mbaya. Unapocheza na timu kama Simba ni lazima wachezaji wawe vizuri kichwani kiakili, huwezi tu kusema tunatumia mfumo huu, sijui nini, ni lazima uwaweke wachezaji wako vizuri kisaikolojia, kwa sababu wanaweza wakaingia wakafanya kitu hicho kikawaondoa kwenye mchezo moja kwa moja," alisema kocha huyo

Aliongeza anaamini katika mchezo huo Pamba Jiji inaweza kupata ushindi wa kwanza nyumbani kutokana na maandalizi na maboresho ambayo wamefanya ndani ya kikosi chao

Pamba Jiji imeshinda mechi moja tu msimu huu ambapo ilikuwa ugenini dhidi ya Fountain Gate, ikiwafunga mabao 3-1, mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Tanzanite Kwaraa mkoani, Manyara

Katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Pamba Jiji iko kwenye nafasi ya 15, ikiwa na pointi nane, baada ya michezo 11, ikishinda mmoja, sare tano na kupoteza michezo mitano

IPP Media

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
58m ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
10h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’