Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' imeweka hai matumaini ya kufuzu fainali za Afcon 2025 ikiibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Ethiopia katika mchezo uliopigwa Kinshasa, DR Congo
Alikuwa ni Saimon Msuva aliyeitanguliza Tanzania kwa bao la kichwa dakika 15 akimalizia mpira wa kona uliopigwa Novutus Dismas
Ikicheza kwa kujiamini na kutawala mchezo katika kipindi cha kwanza, Stars iliongeza bao la pili katika dakika 31 likifungwa Feisal Salum akimalizia pasi nzuri kutoka kwa Mudathir Yahya
Baada ya kwenda mapumziko na uongozi wa mabao 2-0, kipindi cha pili Stars ilicheza kwa tahadhari zaidi ili kulinda uongozi na hatimaye kufanikiwa kuibuka na ushindi
Ni matokeo ambayo yameirejesha Stars nafasi ya pili kundi H baada ya kufikisha alama 7 ikiwa ni kabla ya mchezo kati ya Guinea dhidi ya DR Congo
Tanzania sasa inahitaji kushinda mchezo kuhitimisha hatua ya makundi Novemba 19 dhidi ya Guinea uwanja wa Benjamin Mkapa