Mshambuliaji wa Manchester City, Erling Haaland alifunga hat-trick na kuisaidia Norway kuongoza Kundi B3 katika Ligi ya Mataifa baada ya kushinda 5-0 dhidi ya Kazakhstan Jumapili
Haijalishi jezi gani Erling Haaland anavaa lakini magoli ni uhakika. Fowadi huyo wa Man City aliendelea na kiwango chake cha moto katika Ligi ya Mataifa Jumapili alipofunga mabao matatu katika ushindi wa Norway dhidi ya Kazakhstan kwa mabao 5-0 na kumaliza kileleni mwa Kundi B3 mbele ya Austria ambao walitoka sare ya 1-1 na Slovenia
Haaland alikuwa katika kiwango bora zaidi alipofunga bao maridhawa, akipiga shuti la chini dakika ya 23. Kisha akafunga bao lake la 37 la kimataifa dakika 14 baadaye kutokana na mpira kutoka kwa Antonio Nusa
Mchezaji huyo wa zamani wa Borussia Dortmund alikamilisha bao la tatu na nne kwa Norway zikiwa zimesalia dakika 19 za mchezo
Katika mechi 20 za klabu na timu ya Taifa, Haaland amefunga jumla ya mabao 22



