Local,Normal News,anga

Ramovic ameanza kazi Yanga

Joel JJ By Joel JJ
β€’
18 Nov 2024
Ramovic ameanza kazi Yanga

Baada ya mapumziko ya mwishoni mwa wiki, kikosi cha Yanga kinarejea mazoezini kuendelea na maandalizi ya mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Al Hilal utakaopigwa Jumanne, Novemba 26 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Yanga inarudi mazoezini ikiwa na mabadiliko ya benchi la ufundi ambapo itakuwa siku ya kwanza kazini kwa Kocha Mkuu Sead Ramovic pamoja na kocha msaidizi Mustafa Kodro sambamba na Abdihamid Moallin aliyekuwa kocha wa KMC ambaye kapewa majukumu mapya ya Mkurugenzi wa ufundi

Kocha aliyesitishiwa mkataba Miguel Gamondi alisimamia mazoezi ya timu hiyo wiki iliyopita hadi siku ya Alhamisi pale uongozi ulipofikia uamuzi wa kusitisha mkataba wake na kumtangaza Ramovic aliyetua kutoka klabu ya TS Galaxy ya Afrika Kusini

Baada ya kutambulishwa, Ramovic hakuwa na muda wa kupoteza kwani mwishoni mwa wiki alifanya vikao na uongozi pamoja na benchi la ufundi pia akipata nafasi ya kuifahamu Yanga kwa undani ikiwa ni pamoja na kutazama mechi mbalimbali ambazo Yanga imecheza msimu huu

Kocha huyo raia wa Ujerumani atakuwa na wiki moja ya kukiandaa kikosi chake kabla ya mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Al Hilal utakaopigwa Jumanne, Novemba 26

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’