Ramovic ameanza kazi Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 18th November 2024


Ramovic ameanza kazi Yanga

Baada ya mapumziko ya mwishoni mwa wiki, kikosi cha Yanga kinarejea mazoezini kuendelea na maandalizi ya mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Al Hilal utakaopigwa Jumanne, Novemba 26 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Yanga inarudi mazoezini ikiwa na mabadiliko ya benchi la ufundi ambapo itakuwa siku ya kwanza kazini kwa Kocha Mkuu Sead Ramovic pamoja na kocha msaidizi Mustafa Kodro sambamba na Abdihamid Moallin aliyekuwa kocha wa KMC ambaye kapewa majukumu mapya ya Mkurugenzi wa ufundi

Kocha aliyesitishiwa mkataba Miguel Gamondi alisimamia mazoezi ya timu hiyo wiki iliyopita hadi siku ya Alhamisi pale uongozi ulipofikia uamuzi wa kusitisha mkataba wake na kumtangaza Ramovic aliyetua kutoka klabu ya TS Galaxy ya Afrika Kusini

Baada ya kutambulishwa, Ramovic hakuwa na muda wa kupoteza kwani mwishoni mwa wiki alifanya vikao na uongozi pamoja na benchi la ufundi pia akipata nafasi ya kuifahamu Yanga kwa undani ikiwa ni pamoja na kutazama mechi mbalimbali ambazo Yanga imecheza msimu huu

Kocha huyo raia wa Ujerumani atakuwa na wiki moja ya kukiandaa kikosi chake kabla ya mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Al Hilal utakaopigwa Jumanne, Novemba 26


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.