Bao alilofunga juzi katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za Afcon 2025 dhidi ya Ethiopia, limemfanya winga Saimon Msuva kufikisha mabao 23 akiwa katika jezi ya timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars'
Msuva sasa amebakisha mabao mawili kumfikia mfungaji bora wa muda wote katika timu ya Taifa ya Tanzani, Mrisho Ngasa

Unaweza kusema ni suala la muda tu kwa Msuva kuvunja rekodi hiyo kwani bado ana misimu kadhaa mbele kuendelea kuitumikia Stars kama ataendelea kuwa katika ubora wake
Aidha nahodha wa Stars Mbwana Samatta nae hayuko mbali na rekodi hiyo, yeye akiwa amefunga mabao 22
Kesho Jumanne, Novemba 19 Stars itashuka uwanja wa Benjamin Mkapa kuikabili Guinea katika mchezo wa kuhitimisha hatua ya makundi
Tanzania inahitaji kushinda mchezo huo ili kukata tiketi ya michuano hiyo itakayofanyika nchini Morocco mwakani
Pengine itakuwa nafasi kwa Msuva na Samatta kuikaribia zaidi rekodi ya Ngasa iliyodumu kwa muda mrefu



