Local,Normal News,Yanga, Tanzania

Msuva aikaribia rekodi ya Ngasa

Joel JJ By Joel JJ
β€’
18 Nov 2024
Msuva aikaribia rekodi ya Ngasa

Bao alilofunga juzi katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za Afcon 2025 dhidi ya Ethiopia, limemfanya winga Saimon Msuva kufikisha mabao 23 akiwa katika jezi ya timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars'

Msuva sasa amebakisha mabao mawili kumfikia mfungaji bora wa muda wote katika timu ya Taifa ya Tanzani, Mrisho Ngasa

Unaweza kusema ni suala la muda tu kwa Msuva kuvunja rekodi hiyo kwani bado ana misimu kadhaa mbele kuendelea kuitumikia Stars kama ataendelea kuwa katika ubora wake

Aidha nahodha wa Stars Mbwana Samatta nae hayuko mbali na rekodi hiyo, yeye akiwa amefunga mabao 22

Kesho Jumanne, Novemba 19 Stars itashuka uwanja wa Benjamin Mkapa kuikabili Guinea katika mchezo wa kuhitimisha hatua ya makundi

Tanzania inahitaji kushinda mchezo huo ili kukata tiketi ya michuano hiyo itakayofanyika nchini Morocco mwakani

Pengine itakuwa nafasi kwa Msuva na Samatta kuikaribia zaidi rekodi ya Ngasa iliyodumu kwa muda mrefu

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
58m ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
10h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’