Mshambuliaji Fahad Bayo raia wa Uganda amepata nafasi ya kujifua na kikosi cha Yanga ambapo kama benchi la ufundi litaridhika nae, anaweza kusajiliwa na mabingwa hao wa Tanzania Bara, imefahamika
Bayo ni mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba katika klabu ya MFK Vyskov inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza nchini Czech
Bayo aliitumikia MFK Vyskov katika mechi 42 akifunga mabao nane kutoa pasi moja ya bao
Mshambuliaji huyo ambaye pia ameitumikia timu ya Taifa ya Uganda, ana uzoefu mkubwa katika soka la Kimataifa akicheza klabu kadhaa barani Ulaya
Katika timu ya taifa ya Uganda, Bayo amecheza mechi 21 na kuhusika na mabao tisa, akifunga mabao manane (8) na kupiga pasi moja ya mwisho.
Baadhi ya klabu alizowahi kucheza ndani ya nje ya Afrika ni pamoja na MFK Vyskov (Czech), FC Ashdod (Israel), Bnei Sakhnin (Israel), Buildcon FC (Zambia), Vipers (Uganda) na Proline (Uganda)
Yanga imedhamiria kuongeza mshambuliaji katika dirisha dogo la usajili litakalofunguliwa Disemba 16 2024
Uamuzi huo umewaweka matatani washambuliaji wa kigeni Prince Dube, Kennedy Musonda na Jean Baleke ambao pengine mmoja kati yao anaweza kuondoka dirisha dogo



