Local,Normal News,Yanga, Tanzania

Nitaifikia rekodi ya Ngasa Stars - Msuva

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Nov 2024
Nitaifikia rekodi ya Ngasa Stars - Msuva

Baada ya kufunga bao pekee lililoipeleka Tanzania katika Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2025), zitakazofanyika mwakani nchini Morocco, na kufikisha idadi ya mabao 24, winga, Simon Msuva, amesema ataifikia rekodi ya kupachika mabao mengi kwa timu ya Taifa

Bao hilo lililofungwa na Msuva juzi lilifanya afikishe mabao 24, moja nyuma ya kinara, Mrisho Ngasa

Akizungumza baada ya mchezo huo, Msuva alisema kwa msaada wa Mungu anaweza akaifikia rekodi ya Ngasa kama atakuwa sehemu ya kikosi cha Stars kitakachoshiriki fainali hizo

"Kwanza namshukuru Mungu kutuwezesha kufuzu AFCON, cha kwanza ilikuwa kufuzu kabla ya kuangalia rekodi binafsi, naamini kwenye fainali zijazo naweza kufikia rekodi ya kaka yangu Ngasa," alisema Msuva

Alisema ushindi walioupata ni kwa ajili ya watanzania wote lakini rasmi anaupeleka kwa walioathirika na ajali ya kuporomoka ya ghorofa yalitokea Kariakoo hapa jijini

"Ushindi huu ni kwa ajili yao, kwa pamoja tunahuzunika na kile kilichotokea kwa wenzetu Kariakoo, natoa pole lakini goli nililofunga nalitoa kwa ajili yao," alisema Msuva

Nahodha wa timu hiyo, Mbwana Samatta, anashika nafasi ya tatu akiwa na mabao 22

IPP Media

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
9h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
10h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
14h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
15h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
17h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
21h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’