Makocha Pamba Jiji, Simba watambiana

Joel JJ By Joel JJ β€’ 21st November 2024


Makocha Pamba Jiji, Simba watambiana

Baada ya wiki mbili za mapumziko ya kalenda ya FIFA, Ligi Kuu ya NBC inarejea kesho Ijumaa ambapo mchezo mmoja kati ya Pamba Jiji dhidi ya Simba utapigwa uwanja wa CCM Kirumba

Wakizungumza katika Mkutano na Wanahabari mapema leo, makocha wa timu hizo Fred Felix Minziro (Pamba Jiji) na Fadlu Davids (Simba) wametamba timu zao kupata matokeo mazuri katika mchezo huo

Kocha Mkuu wa Simba Fadlu amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo huo wakiwa na malengo ya kuondoka na alama zote tatu

Licha ya ratiba ya mchezo huo kuwa ni siku chache baada ya mechi za Kimataifa katika kalenda ya FIFA, Fadlu amesema hakuna athari zozote katika maandalizi kwani wachezaji wake waliokuwa timu za Taifa, wametumika

"Tuko hapa Mwanza wachezaji wakiwa na ari na morali kubwa kuelekea mchezo wa kesho dhidi ya Pamba Jiji. Tumekuwa na maandalizi mazuri kuelekea mchezo huu"

"Ratiba ya mechi za kalenda ya FIFA haijatuathiri kwa sababu wachezaji wengi wametumika katika timu zao za Taifa"

"Wachezaji wako timamu kimwili na kiakili kuelekea mchezo dhidi ya Pamba Jiji hapo kesho," alisema Fadlu

Nae Minziro ambaye aliingoza Pamba Jiji kupata ushindi wa kwanza msimu huu kwa kuichapa Fountain Gate mabao 3-1 kabla ya mapumziko ya kalenda ya FIFA, amesema amepata muda mzuri wa kufanya maandalizi hivyo wakazi wa Mwanza watarajie timu yao kupata matokeo mazuri katika mchezo dhidi ya Simba

"Nimefurahi, nimepata muda wa kutosha wa kufanya maandalizi, kuwasoma wachezaji wangu na kufanya marekebisho muhimu. Niseme tu kesho mashabiki wetu watarajie kupata burudani,"alisema Minziro

Simba iko kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa imekusanya alama 25 kutoka mechi 10 wakati Pamba Jiji wanashika nafasi ya 15 wakiwa na alama 8


  

More Stories

Yanga yarejea kileleni Ligi Kuu ikiibamiza Fountain Gate 2-0
Yanga yarejea kileleni Ligi Kuu ikiibamiza Fountain Gate 2-0
Today, READ MORE β†’
Kane aifikia rekodi ya Lineker ya mabao 10 kombe la Dunia
Kane aifikia rekodi ya Lineker ya mabao 10 kombe la Dunia
Today, READ MORE β†’
Simba yalimwa faini 10M, Mabena, Komba wakumbana na rungu la kamati ya saa 72
Simba yalimwa faini 10M, Mabena, Komba wakumbana na rungu la kamati ya saa 72
Today, READ MORE β†’
Simba yamfuatilia kipa wa Zimbabwe Nelson Chadya
Simba yamfuatilia kipa wa Zimbabwe Nelson Chadya
Today, READ MORE β†’
Zwane kukosa mechi zilizobaki kombe la Dunia
Zwane kukosa mechi zilizobaki kombe la Dunia
Today, READ MORE β†’
Sowah kurejea Singida BS?
Sowah kurejea Singida BS?
Today, READ MORE β†’
Mubiru atua Azam Fc
Mubiru atua Azam Fc
Today, READ MORE β†’
Ligi Kuu: Yanga mikononi mwa Fountain Gate, mechi tatu kupigwa leo
Ligi Kuu: Yanga mikononi mwa Fountain Gate, mechi tatu kupigwa leo
Today, READ MORE β†’
Ghana yaandikisha ushindi wa pili kwa Afrika, Uingereza yaanza kwa kishindo
Ghana yaandikisha ushindi wa pili kwa Afrika, Uingereza yaanza kwa kishindo
Today, READ MORE β†’
DR Congo yapata sare ya kihistoria kombe la Dunia
DR Congo yapata sare ya kihistoria kombe la Dunia
Today, READ MORE β†’