Local,Normal News,Pamba, Simba

Makocha Pamba Jiji, Simba watambiana

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Nov 2024
Makocha Pamba Jiji, Simba watambiana

Baada ya wiki mbili za mapumziko ya kalenda ya FIFA, Ligi Kuu ya NBC inarejea kesho Ijumaa ambapo mchezo mmoja kati ya Pamba Jiji dhidi ya Simba utapigwa uwanja wa CCM Kirumba

Wakizungumza katika Mkutano na Wanahabari mapema leo, makocha wa timu hizo Fred Felix Minziro (Pamba Jiji) na Fadlu Davids (Simba) wametamba timu zao kupata matokeo mazuri katika mchezo huo

Kocha Mkuu wa Simba Fadlu amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo huo wakiwa na malengo ya kuondoka na alama zote tatu

Licha ya ratiba ya mchezo huo kuwa ni siku chache baada ya mechi za Kimataifa katika kalenda ya FIFA, Fadlu amesema hakuna athari zozote katika maandalizi kwani wachezaji wake waliokuwa timu za Taifa, wametumika

"Tuko hapa Mwanza wachezaji wakiwa na ari na morali kubwa kuelekea mchezo wa kesho dhidi ya Pamba Jiji. Tumekuwa na maandalizi mazuri kuelekea mchezo huu"

"Ratiba ya mechi za kalenda ya FIFA haijatuathiri kwa sababu wachezaji wengi wametumika katika timu zao za Taifa"

"Wachezaji wako timamu kimwili na kiakili kuelekea mchezo dhidi ya Pamba Jiji hapo kesho," alisema Fadlu

Nae Minziro ambaye aliingoza Pamba Jiji kupata ushindi wa kwanza msimu huu kwa kuichapa Fountain Gate mabao 3-1 kabla ya mapumziko ya kalenda ya FIFA, amesema amepata muda mzuri wa kufanya maandalizi hivyo wakazi wa Mwanza watarajie timu yao kupata matokeo mazuri katika mchezo dhidi ya Simba

"Nimefurahi, nimepata muda wa kutosha wa kufanya maandalizi, kuwasoma wachezaji wangu na kufanya marekebisho muhimu. Niseme tu kesho mashabiki wetu watarajie kupata burudani,"alisema Minziro

Simba iko kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa imekusanya alama 25 kutoka mechi 10 wakati Pamba Jiji wanashika nafasi ya 15 wakiwa na alama 8

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
8h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
10h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
14h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
15h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
17h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
20h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’