Kiungo wa zamani wa Chelsea na Leicester City raia wa Uingereza Dani Drinkwater ambaye alishinda ubingwa EPL akiwa na Leicester City mwaka wa 2016, sasa ni mtaalam wa ujenzi
Baada ya kuitumikia Leicester City kwa mafanikio, Drinkwater alisajiliwa na Chelsea mwaka wa 2017 kabla ya kutolewa kwa mkopo katika klabu ya Burnley
Kandarasi yake na Chelsea ilifikia ukomo Juni 2022 ambapo mchezaji huyo hakuweza kupata klabu mpya, alitangaza kustaafu soka la kulipwa mnamo Mei 2023
Drinkwater sasa anafanya kazi katika ujenzi. Katika mahojiano na The Telegraph, alitaja kufurahia kazi anayoifanya kwa sasa




