International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Novemba 23 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 Nov 2024
Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Novemba 23 2024

Mshambuliaji wa Ipswich Muingereza Liam Delap, 21, anasakwa na Chelsea baada ya klabu hiyo kusitisha mpango wa kumnunua mshambuliaji wa Newcastle na Uswidi Alexander Isak, 25. (I - usajili unahitajika)

Arsenal, huenda wakajaribu kumshawishi Isak kuhamia Uwanja wa Emirates mwezi Januari kwa ofa ya kucheza Ligi ya Mabingwa. (Give Me Sport)

Mshambuliaji wa Ufaransa Christopher Nkunku hana furaha kutokana na kukosa muda wa kuchezea Chelsea lakini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 hana mpango wa kuondoka Stamford Bridge kwa sasa. (Athletic-Usajili unahitajika)

Liverpool wanatarajiwa kufanya jaribio la pili la kumnunua kiungo wa Real Sociedad Martin Zubimendi, 25, mwezi Januari lakini watakabiliwa na ushindani kutoka kwa Arsenal kumnunua mchezaji huyo wa kimataifa wa Uhispania. (Team Talk)

Newcastle wanawafuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 21, na mchezaji wa kimataifa wa Canada Jonathan David David wa Lille, 24 wakati wakitathmini uwezekano wa kumnunua kiungo mshambuliaji mwezi Januari. (The I -usajili unahitajika)

Wakuu wa Manchester United wana mashaka na mchezo wa mshambuliaji wa Uholanzi Joshua Zirkzee, 23, tangu alipomnunua kwa £36.5m kutoka Bologna msimu wa joto. (Manchester Evening News)

Tottenham wana matumaini ya kuwashinda Manchester United na Newcastle mbio za kumsaini ya kiungo wa kati wa Lille na Uingereza Angel Gomes, 24. (GiveMeSport)

Winga wa Uhispania Lamine Yamal, 17, amekubali kusaini mkataba mpya wa miaka sita katika klabu ya Barcelona atakapofikisha umri wa miaka 18. (El Chiringuito TV, via Football Espana)

Kocha mkuu wa Sunderland Regis Le Bris anataka viungo wa kati wa Uingereza Jobe Bellingham, 19, na Chris Rigg, 17, kusalia katika Stadium Of Light ili kuendeleza fani yao ya soka huku klabu kadhaa za Ligi ya Premia zikiwanyatia. (Sunderland Echo)

Galatasaray wanamfuatilia mlinda lango wa Liverpool na Brazil Alisson Becker, 32, huku wakimtafuta atakayechukua nafasi ya Fernando Muslera, 38, wa Uruguay, mwishoni mwa msimu huu. (Sabah - kwa Kituruki)

Manchester City wameelekeza darubini yao kwa winga wa Sporting na Uruguay Maximiliano Araujo, 24. (Football Insider)

Newcastle wako katika nafasi nzuri ya kumsajili mshambuliaji wa Algeria Ibrahim Maza, 18, baada ya Hertha Berlin kupunguza bei yake hadi euro milioni 20. (Caught Offside)

Tottenham wanatazamiwa kukabiliwa na ushindani kutoka kwa Atletico Madrid kumnunua kiungo wa Real Betis na Marekani Johnny Cardoso, 23. (Estadio Deportivo - kwa Kihispania)

Mlinzi wa Slovakia Milan Skriniar, 29, anataka kuondoka Paris St-Germain mwezi Januari baada ya kukosa nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza, huku klabu kadhaa za Ligi Kuu ya England zikifuatilia hali yake. Juventus na Napoli pia wanamtaka. (Le Parisien - kwa Kifaransa)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
2h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
3h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
4h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
4h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
5h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
20h ago
READ MORE β†’