Mchezo wa Ligi Kuu Bara kati ya Tabora United dhidi ya Singida Black Stars uliokuwa uchezwe jana Novemba 24 kwenye Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi Tabora uliahirishwa baada ya mvua kubwa kunyesha na kusababisha uwanja kujaa maji
Kutokana na kadhia hiyo, mchezo huo umepagwa kuchezwa leo Jumatatu Novemba 25, 2024 saa 4:00 asubuhi
Kamishna kutoka Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Said Mkai amesema walifanya jitihada za kuhakikisha mchezo huo unachezwa jana lakini ilishindikana
Mkai alibainisha makubaliano ya mchezo huo kuahirishwa yalifikiwa kwa timu zote mbili kushirikishwa na kuamua uahirishwe



