Yanga yakamilisha maandalizi kuikabili Al Hilal

Joel JJ By Joel JJ β€’ 25th November 2024


Yanga yakamilisha maandalizi kuikabili Al Hilal

Kikosi cha Yanga leo kimefanya mazoezi yake ya mwisho katika uwanja wa Benjamin Mkapa kuelekea mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika

Kesho Jumanne, Novemba 26 Yanga itakuwa mwenyeji wa Al Hilal katika mchezo utakaopigwa dimba la Mkapa, saa 10 jioni

Kocha mpya wa Yanga Sead Ramovic aliongoza mazoezi ya kikosi chake leo ikiwa ni siku ya nane tangu alipotangazwa kuchukua mikoba ya Miguel Gamondi ambaye wiki iliyopita, alionyeshwa mlango wa kutokea

Wapinzani wao Al Hilal wako nchini tangu wiki iliyopita, jioni watajifua katika uwanja wa Benjamin Mkapa


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.