Kikosi cha Yanga leo kimefanya mazoezi yake ya mwisho katika uwanja wa Benjamin Mkapa kuelekea mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika
Kesho Jumanne, Novemba 26 Yanga itakuwa mwenyeji wa Al Hilal katika mchezo utakaopigwa dimba la Mkapa, saa 10 jioni
Kocha mpya wa Yanga Sead Ramovic aliongoza mazoezi ya kikosi chake leo ikiwa ni siku ya nane tangu alipotangazwa kuchukua mikoba ya Miguel Gamondi ambaye wiki iliyopita, alionyeshwa mlango wa kutokea
Wapinzani wao Al Hilal wako nchini tangu wiki iliyopita, jioni watajifua katika uwanja wa Benjamin Mkapa



